Swahili
Sorah Al-'alaq ( The Clot ) - Verses Number 19
اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ 
( 1 )  
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
خَلَقَ الْإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ 
( 2 )  
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ 
( 3 )  
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ 
( 4 )  
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
عَلَّمَ الْإِنسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ 
( 5 )  
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
كَلَّا إِنَّ الْإِنسَانَ لَيَطْغَىٰ 
( 6 )  
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
أَن رَّآهُ اسْتَغْنَىٰ 
( 7 )  
Akijiona katajirika.
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ الرُّجْعَىٰ 
( 8 )  
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
أَرَأَيْتَ الَّذِي يَنْهَىٰ 
( 9 )  
Umemwona yule anaye mkataza
عَبْدًا إِذَا صَلَّىٰ 
( 10 )  
Mja anapo sali?
أَرَأَيْتَ إِن كَانَ عَلَى الْهُدَىٰ 
( 11 )  
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
أَوْ أَمَرَ بِالتَّقْوَىٰ 
( 12 )  
Au anaamrisha uchamngu?
أَرَأَيْتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ 
( 13 )  
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
أَلَمْ يَعْلَم بِأَنَّ اللَّهَ يَرَىٰ 
( 14 )  
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
كَلَّا لَئِن لَّمْ يَنتَهِ لَنَسْفَعًا بِالنَّاصِيَةِ 
( 15 )  
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
نَاصِيَةٍ كَاذِبَةٍ خَاطِئَةٍ 
( 16 )  
Shungi la uwongo, lenye makosa!
فَلْيَدْعُ نَادِيَهُ 
( 17 )  
Basi na awaite wenzake!
سَنَدْعُ الزَّبَانِيَةَ 
( 18 )  
Nasi tutawaita Mazabania!
كَلَّا لَا تُطِعْهُ وَاسْجُدْ وَاقْتَرِب ۩ 
( 19 )  
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!