Swahili
Sorah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Verses Number 26
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ 
( 1 )  
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ 
( 2 )  
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ 
( 3 )  
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً 
( 4 )  
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ 
( 5 )  
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ 
( 6 )  
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِن جُوعٍ 
( 7 )  
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ 
( 8 )  
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ 
( 9 )  
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ 
( 10 )  
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً 
( 11 )  
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ 
( 12 )  
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ 
( 13 )  
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ 
( 14 )  
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ 
( 15 )  
Na matakia safu safu,
وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ 
( 16 )  
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ 
( 17 )  
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ 
( 18 )  
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ 
( 19 )  
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ 
( 20 )  
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ 
( 21 )  
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ 
( 22 )  
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ 
( 23 )  
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ 
( 24 )  
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ 
( 25 )  
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم 
( 26 )  
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!