Swahili
Sorah Al-Qiyamah ( The Resurrection ) - Verses Number 40
لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ 
( 1 )  
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ 
( 2 )  
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُ 
( 3 )  
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
بَلَىٰ قَادِرِينَ عَلَىٰ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُ 
( 4 )  
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ 
( 5 )  
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ 
( 6 )  
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ 
( 7 )  
Basi jicho litapo dawaa,
وَخَسَفَ الْقَمَرُ 
( 8 )  
Na mwezi utapo patwa,
وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ 
( 9 )  
Na likakusanywa jua na mwezi,
يَقُولُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ 
( 10 )  
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
كَلَّا لَا وَزَرَ 
( 11 )  
La! Hapana pa kukimbilia!
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمُسْتَقَرُّ 
( 12 )  
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
يُنَبَّأُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ 
( 13 )  
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
بَلِ الْإِنسَانُ عَلَىٰ نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ 
( 14 )  
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُ 
( 15 )  
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ 
( 16 )  
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ 
( 17 )  
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ 
( 18 )  
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ 
( 19 )  
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ 
( 20 )  
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ 
( 21 )  
Na mnaacha maisha ya Akhera.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ 
( 22 )  
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ 
( 23 )  
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ 
( 24 )  
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ 
( 25 )  
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
كَلَّا إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِيَ 
( 26 )  
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ 
( 27 )  
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ 
( 28 )  
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ 
( 29 )  
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ 
( 30 )  
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ 
( 31 )  
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ 
( 32 )  
Bali alikanusha, na akageuka.
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰ أَهْلِهِ يَتَمَطَّىٰ 
( 33 )  
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ 
( 34 )  
Ole wako, ole wako!
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ 
( 35 )  
Kisha Ole wako, ole wako!
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى 
( 36 )  
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَىٰ 
( 37 )  
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ 
( 38 )  
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ 
( 39 )  
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ 
( 40 )  
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?