Swahili
Sorah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Verses Number 25
إِذَا السَّمَاءُ انشَقَّتْ 
( 1 )  
Itapo chanika mbingu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ 
( 2 )  
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ 
( 3 )  
Na ardhi itakapo tanuliwa,
وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ 
( 4 )  
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ 
( 5 )  
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ 
( 6 )  
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ 
( 7 )  
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا 
( 8 )  
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا 
( 9 )  
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ 
( 10 )  
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا 
( 11 )  
Basi huyo ataomba kuteketea.
وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا 
( 12 )  
Na ataingia Motoni.
إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا 
( 13 )  
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
إِنَّهُ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ 
( 14 )  
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا 
( 15 )  
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ 
( 16 )  
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ 
( 17 )  
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ 
( 18 )  
Na kwa mwezi unapo pevuka,
لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍ 
( 19 )  
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ 
( 20 )  
Basi wana nini hawaamini?
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩ 
( 21 )  
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ 
( 22 )  
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ 
( 23 )  
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ 
( 24 )  
Basi wabashirie adhabu chungu!
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ 
( 25 )  
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.