Swahili
Sorah An-Nazi'at ( Those who Pull Out ) - Verses Number 46
وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا 
( 1 )  
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَالنَّاشِطَاتِ نَشْطًا 
( 2 )  
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَالسَّابِحَاتِ سَبْحًا 
( 3 )  
Na wanao ogelea,
فَالسَّابِقَاتِ سَبْقًا 
( 4 )  
Wakishindana mbio,
فَالْمُدَبِّرَاتِ أَمْرًا 
( 5 )  
Wakidabiri mambo.
يَوْمَ تَرْجُفُ الرَّاجِفَةُ 
( 6 )  
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتْبَعُهَا الرَّادِفَةُ 
( 7 )  
Kifuate cha kufuatia.
قُلُوبٌ يَوْمَئِذٍ وَاجِفَةٌ 
( 8 )  
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبْصَارُهَا خَاشِعَةٌ 
( 9 )  
Macho yatainama chini.
يَقُولُونَ أَإِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِي الْحَافِرَةِ 
( 10 )  
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَإِذَا كُنَّا عِظَامًا نَّخِرَةً 
( 11 )  
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُوا تِلْكَ إِذًا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌ 
( 12 )  
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ 
( 13 )  
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِالسَّاهِرَةِ 
( 14 )  
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ مُوسَىٰ 
( 15 )  
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذْ نَادَاهُ رَبُّهُ بِالْوَادِ الْمُقَدَّسِ طُوًى 
( 16 )  
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
اذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُ طَغَىٰ 
( 17 )  
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰ أَن تَزَكَّىٰ 
( 18 )  
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ 
( 19 )  
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَاهُ الْآيَةَ الْكُبْرَىٰ 
( 20 )  
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ 
( 21 )  
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ 
( 22 )  
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ 
( 23 )  
Akakusanya watu akanadi.
فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ 
( 24 )  
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
فَأَخَذَهُ اللَّهُ نَكَالَ الْآخِرَةِ وَالْأُولَىٰ 
( 25 )  
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِّمَن يَخْشَىٰ 
( 26 )  
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
أَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ السَّمَاءُ ۚ بَنَاهَا 
( 27 )  
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّاهَا 
( 28 )  
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَاهَا 
( 29 )  
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
وَالْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَاهَا 
( 30 )  
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
أَخْرَجَ مِنْهَا مَاءَهَا وَمَرْعَاهَا 
( 31 )  
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
وَالْجِبَالَ أَرْسَاهَا 
( 32 )  
Na milima akaisimamisha,
مَتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ 
( 33 )  
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَاءَتِ الطَّامَّةُ الْكُبْرَىٰ 
( 34 )  
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ مَا سَعَىٰ 
( 35 )  
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ 
( 36 )  
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ 
( 37 )  
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
وَآثَرَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا 
( 38 )  
Na akakhiari maisha ya dunia,
فَإِنَّ الْجَحِيمَ هِيَ الْمَأْوَىٰ 
( 39 )  
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ وَنَهَى النَّفْسَ عَنِ الْهَوَىٰ 
( 40 )  
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
فَإِنَّ الْجَنَّةَ هِيَ الْمَأْوَىٰ 
( 41 )  
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا 
( 42 )  
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا 
( 43 )  
Una nini wewe hata uitaje?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَاهَا 
( 44 )  
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
إِنَّمَا أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَاهَا 
( 45 )  
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَاهَا 
( 46 )  
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.