Swahili
Sorah At-Takwir ( The Overthrowing ) - Verses Number 29
إِذَا الشَّمْسُ كُوِّرَتْ 
( 1 )  
Jua litakapo kunjwa,
وَإِذَا النُّجُومُ انكَدَرَتْ 
( 2 )  
Na nyota zikazimwa,
وَإِذَا الْجِبَالُ سُيِّرَتْ 
( 3 )  
Na milima ikaondolewa,
وَإِذَا الْعِشَارُ عُطِّلَتْ 
( 4 )  
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
وَإِذَا الْوُحُوشُ حُشِرَتْ 
( 5 )  
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
وَإِذَا الْبِحَارُ سُجِّرَتْ 
( 6 )  
Na bahari zikawaka moto,
وَإِذَا النُّفُوسُ زُوِّجَتْ 
( 7 )  
Na nafsi zikaunganishwa,
وَإِذَا الْمَوْءُودَةُ سُئِلَتْ 
( 8 )  
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
بِأَيِّ ذَنبٍ قُتِلَتْ 
( 9 )  
Kwa kosa gani aliuliwa?
وَإِذَا الصُّحُفُ نُشِرَتْ 
( 10 )  
Na madaftari yatakapo enezwa,
وَإِذَا السَّمَاءُ كُشِطَتْ 
( 11 )  
Na mbingu itapo tanduliwa,
وَإِذَا الْجَحِيمُ سُعِّرَتْ 
( 12 )  
Na Jahannamu itapo chochewa,
وَإِذَا الْجَنَّةُ أُزْلِفَتْ 
( 13 )  
Na Pepo ikasogezwa,
عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا أَحْضَرَتْ 
( 14 )  
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
فَلَا أُقْسِمُ بِالْخُنَّسِ 
( 15 )  
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
الْجَوَارِ الْكُنَّسِ 
( 16 )  
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
وَاللَّيْلِ إِذَا عَسْعَسَ 
( 17 )  
Na kwa usiku unapo pungua,
وَالصُّبْحِ إِذَا تَنَفَّسَ 
( 18 )  
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ 
( 19 )  
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي الْعَرْشِ مَكِينٍ 
( 20 )  
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
مُّطَاعٍ ثَمَّ أَمِينٍ 
( 21 )  
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجْنُونٍ 
( 22 )  
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
وَلَقَدْ رَآهُ بِالْأُفُقِ الْمُبِينِ 
( 23 )  
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
وَمَا هُوَ عَلَى الْغَيْبِ بِضَنِينٍ 
( 24 )  
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَيْطَانٍ رَّجِيمٍ 
( 25 )  
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
فَأَيْنَ تَذْهَبُونَ 
( 26 )  
Basi mnakwenda wapi?
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ 
( 27 )  
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ 
( 28 )  
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ 
( 29 )  
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.