Swahili
Sorah Al-Mursalat ( Those sent forth ) - Verses Number 50
وَالْمُرْسَلَاتِ عُرْفًا 
( 1 )  
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
فَالْعَاصِفَاتِ عَصْفًا 
( 2 )  
Na zinazo vuma kwa kasi!
وَالنَّاشِرَاتِ نَشْرًا 
( 3 )  
Na zikaeneza maeneo yote!
فَالْفَارِقَاتِ فَرْقًا 
( 4 )  
Na zinazo farikisha zikatawanya!
فَالْمُلْقِيَاتِ ذِكْرًا 
( 5 )  
Na zinazo peleka mawaidha!
عُذْرًا أَوْ نُذْرًا 
( 6 )  
Kwa kuudhuru au kuonya,
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَاقِعٌ 
( 7 )  
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
فَإِذَا النُّجُومُ طُمِسَتْ 
( 8 )  
Wakati nyota zitakapo futwa,
وَإِذَا السَّمَاءُ فُرِجَتْ 
( 9 )  
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا الْجِبَالُ نُسِفَتْ 
( 10 )  
Na milima itakapo peperushwa,
وَإِذَا الرُّسُلُ أُقِّتَتْ 
( 11 )  
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
لِأَيِّ يَوْمٍ أُجِّلَتْ 
( 12 )  
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
لِيَوْمِ الْفَصْلِ 
( 13 )  
Kwa siku ya kupambanua!
وَمَا أَدْرَاكَ مَا يَوْمُ الْفَصْلِ 
( 14 )  
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 15 )  
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نُهْلِكِ الْأَوَّلِينَ 
( 16 )  
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
ثُمَّ نُتْبِعُهُمُ الْآخِرِينَ 
( 17 )  
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ 
( 18 )  
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 19 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نَخْلُقكُّم مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ 
( 20 )  
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
فَجَعَلْنَاهُ فِي قَرَارٍ مَّكِينٍ 
( 21 )  
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
إِلَىٰ قَدَرٍ مَّعْلُومٍ 
( 22 )  
Mpaka muda maalumu?
فَقَدَرْنَا فَنِعْمَ الْقَادِرُونَ 
( 23 )  
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 24 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ كِفَاتًا 
( 25 )  
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
أَحْيَاءً وَأَمْوَاتًا 
( 26 )  
Walio hai na maiti?
وَجَعَلْنَا فِيهَا رَوَاسِيَ شَامِخَاتٍ وَأَسْقَيْنَاكُم مَّاءً فُرَاتًا 
( 27 )  
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 28 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
انطَلِقُوا إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ 
( 29 )  
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
انطَلِقُوا إِلَىٰ ظِلٍّ ذِي ثَلَاثِ شُعَبٍ 
( 30 )  
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
لَّا ظَلِيلٍ وَلَا يُغْنِي مِنَ اللَّهَبِ 
( 31 )  
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
إِنَّهَا تَرْمِي بِشَرَرٍ كَالْقَصْرِ 
( 32 )  
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
كَأَنَّهُ جِمَالَتٌ صُفْرٌ 
( 33 )  
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 34 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
هَٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ 
( 35 )  
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ 
( 36 )  
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 37 )  
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ ۖ جَمَعْنَاكُمْ وَالْأَوَّلِينَ 
( 38 )  
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
فَإِن كَانَ لَكُمْ كَيْدٌ فَكِيدُونِ 
( 39 )  
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 40 )  
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي ظِلَالٍ وَعُيُونٍ 
( 41 )  
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
وَفَوَاكِهَ مِمَّا يَشْتَهُونَ 
( 42 )  
Na matunda wanayo yapenda,
كُلُوا وَاشْرَبُوا هَنِيئًا بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ 
( 43 )  
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ 
( 44 )  
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 45 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
كُلُوا وَتَمَتَّعُوا قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجْرِمُونَ 
( 46 )  
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 47 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ارْكَعُوا لَا يَرْكَعُونَ 
( 48 )  
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ 
( 49 )  
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
فَبِأَيِّ حَدِيثٍ بَعْدَهُ يُؤْمِنُونَ 
( 50 )  
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?